MIMP YAPOKEA MELI KUBWA YA KITALII “THE WORLD CRUISE” ILIYOBEBA WATU 442

08 Apr, 2024 09:30AM-05:40PM MAFIA
MIMP YAPOKEA MELI KUBWA YA KITALII “THE WORLD CRUISE” ILIYOBEBA WATU 442

Meli kubwa ya kitalii iliyobeba jumla ya watu 442 imetia nanga katika Hifadhi ya Bahari ya Bahari ya Kisiwa cha Mafia (MIMP) iliyopo katika Wilaya ya Mafia ikitokea Moroni, Visiwa vya Comoro.

Meli hiyo ijulikanayo kama "The World " yenye wahudumu wapatao 288 ( crew) na abiria 154 imefika katika eneo la Ras Kisimani Mafia ambapo watalii waliweza kupata burudani kutoka kwa vikundi mbalimbali vya ngoma za asili na kujionea mandhari nzuri.