MPRU YAPIGA HATUA UHIFADHI WA MIAMBA YA MATUMBAWE
MPRU YAPIGA HATUA UHIFADHI WA MIAMBA YA MATUMBAWE

Jumanne, Mei 26, 2026, Kibaha - Dar es Salaam

                                                                                                                                              

Tanzania inaendelea kufanya vizuri katika juhudi za kulinda miamba ya matumbawe dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi kupitia Mradi wa Global Environment Facility–Coral Reef Rescue Initiative (GEF-CRRI), unaolenga kuhifadhi mifumo ikolojia ya baharini muhimu kwa bioanuwai na maisha ya jamii za mwambao.

Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Kitaifa ya Uongozi wa mradi huo kilichofanyika Kibaha, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) na Meneja wa Mradi, Bw. Godfrey Ngupula, alisema mradi huo unatekelezwa wakati dunia ikikabiliwa na changamoto kubwa za uharibifu wa mazingira unaochochewa na mabadiliko ya tabianchi.

Alisema mradi huo wa miaka minne wenye thamani ya dola za Marekani 900,000 uliozinduliwa mwaka 2023 chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais, unalenga kukabiliana na athari za tabianchi kwa kuhifadhi na kusimamia kwa uendelevu miamba ya matumbawe.

Bw. Ngupula alieleza kuwa tafiti zinaonyesha baadhi ya matumbawe yaliyopo Tanzania yana uwezo mkubwa wa kustahimili ongezeko la joto na uchafuzi wa mazingira, lakini hatua za makusudi za uhifadhi zinahitajika ili kuhakikisha yanaendelea kuwepo kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Kwa upande wake, Mratibu wa Programu wa Shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani (WWF), Dkt. Modesta Medard, alisema Tanzania imepiga hatua muhimu katika utekelezaji wa mradi huo ikiwemo kuanzisha Kituo cha Kitaifa cha Miamba ya Matumbawe (NCRH), kurejesha maeneo yaliyoharibika na kuimarisha ushirikiano wa wadau kupitia miongozo maalum.

Naye, Meneja wa MPRU, Dkt. Emmanuel Andrew Sweke, alisema mradi huo unaendana na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 na una mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa buluu. Alibainisha kuwa miamba ya matumbawe ni makazi muhimu ya viumbe wa baharini, huku juhudi za urejeshaji zinazoendelea katika eneo la Mnazi Bay zikionyesha mafanikio ya ushirikiano kati ya serikali, wadau na jamii za mwambao.

slot gacor