SIKU YA BAHARI DUNIANI JUNI 8, 2023

11 May, 2023

Tarehe 8 Juni, ulimwengu unajumuika kwa pamoja kusherehekea Siku ya Bahari, tukio maalum kwa ajili ya kuongeza ufahamu kuhusu umuhimu wa bahari zetu na hatua za kuhimiza kuzihifadhi.

Kama taasisi yenye kujihusisha na  uhifadhi wa Bahari na Maeneo yake tengefu, lengo letu kuu liko katika kulinda makazi ya baharini na kuendeleza uhifadhi ndani ya maeneo hayo yaliyotengwa.

Lengo letu kuu ni kufufua na kurejesha mfumo wa kiikolojia wa baharini ambao umeathiriwa vibaya. Ni heshima kubwa kwetu kuadhimisha siku hii tukiungana na jumuiya ya kimataifa kutambua umuhimu wa kihistoria wa bahari zetu na hitaji la dharura la kuzilinda kwa ajili ya vizazi vijavyo.